Friday, November 30, 2012

CHRISC ARUSHA YOUTH LEAGUE FINAL




CHRISC Arusha youth league ni mashindano yanayo andaliwa na CHRISC kila mwaka. Chrisc ina matawi manne ambayo ni Tanga, Mwanza, Manyara, Kilimajaro, na Arusha ambapo ndipo makao makuu ya CHRISC Tanzania.

League hii kwa CHRISC Arusha kwa mwaka huu wa 2012 ili itimishwa tarehe  24/11/2012 ilianza munamo tarehe 10/03/2012. League ya CHRISC kwa mwaka huu ilishirikisha jumla ya team 98. Kwa mujibu wa Rapha Paul ambaye ndiye mratibu wa CHRISC Arusha alisema kuwa team za wasichana zilikuwa 6 na za wavulana  zilikuwa jumla ya team 96  team za wasichana zote zilitoka katika kituo cha Meserani.


CHRISC ARUSHA YOUTH LEAGUE FINAL 2012

Final ya ligi ya CHRISC Arusha kwa mwaka huu kama kawaida ya kila mwaka ilifanyika katika zone moja iliyo jumuisha washindi wa zone zote za CHRISC Arusha. Final hii ilifanyika katika kituo cha Eso almaarufu kama kituo cha Palot ambacho  hufanya shughuli za kaendesha league ya CHRISC.  Timu zilizo fuzu kucheza final ya league ya CHRISC kwa mwaka huu ni pamoja na Tacoda fc kutoka kituo cha kaloleni ambacho kinaendesha ligi katika kiwanja cha Soweto. Yosso united pia kutoka kaloleni under 16, paloti under16 na14 pia kutoka kituo cha Esso, na hardroock kutoka kituo cha Suye na Kijenge youth  na Tiger Boys  kutoka kitio cha Suye



FINAL



CHRISC Arusha kwa mwaka huu kwa final ilianza tarehe 17/11/2012 kwa robo final iliyozikutanisha team kutoka zone zote katika kituo cha Suye. Na team zilizo fuzu final ndizo zilizoshiriki fainal kitika kituo cha Esso. Michezo ya fainali ilianza majira ya saa 3 kamili kwa michezo ya under 12 na mshindi wa umri hii alitoka katika kituo cha Suye kwa team ya Kijenge youth. Baada ya apo ilichezwa fainali ya under 14 iliyo chezwa kati ya team ya Tacoda fc na team kutoka katiki kituo cha Meserani na Tacoda fc waliibuka washindi wa umri huu. Pia baada ya apo ilichezwa mechi ya under 16 iliyozikutanisha team za Hardroock na palot na hatimaye Palot waliibuka washindi wa umri huu. Pia baada ya hapo ilichezwa mechi ya under 17 iliyokutanisha team za Yosso united na Tiger Boys ya kutoka Suye na mshindi wa mechi hii alikua ni timu ya Tiger Boys.



No comments:

Post a Comment